Mtibwa Sugar wakiwa kwenye dimba lao la nyumbani, Manungu Complex, mkoani Morogoro imeitandika Geita Gold 2-0 katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara #NBCPremierleague. Magoli ya Mtibwa yametoka kwa Nzigamasabo Styve dakika 27 na Mululi Mayanja dakika ya 76.