Content removal request!


Magoli na kadi nyekundu | Yanga 4-1 Tanzania Prisons | Azam Sports Federation Cup 03/03/2023

Clement Mzize amehusika kwenye magoli yote manne, Yanga ikiichapa Tanzania Prisons 4-1 katika mchezo wa 16 bora na kutinga robo fainali kwa kishindo. Clement Mzize amefunga magoli magoli dakika ya 70 na 88 huku akisababisha goli la kwanza lililofungwa na Bakari Mwamnyeto dakika ya 52 na penati iliyofungwa na Stephane Aziz Ki dakika ya 69. Katika mchezo huu uliomaliza dakika 45 za kipindi cha kwanza bila goli, Tanzania Prisons walipata pigo kwa beki wake Ibrahim Abraham kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 45 baada ya kupata njano mbili, lakini pia Clement Mzize alikosa penati dakika ya 90. Ni #AzamSportsFederationCup iliyopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.