Content removal request!


Magoli yote: Ndanda SC 3-0 Mwadui FC (VPL 23/05/2018)

Ni mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Ndanda SC na Mwadui FC inayopigwa dimba la Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, ambapo hadi kipindi cha kwanza kinamalizika, Ndanda walikuwa mbele kwa mabao 3-0. Ndanda FC ambayo inapigania kutoshuka daraja, imeanza kwa kasi na kujipatia magoli matatu ndani ya kipindi cha kwanza kupitia kwa Jacob Massawe dakika ya 3, Mrisho Ngassa dakika ya 5 na Tibar John dakika ya 40. Mabao hayo yamedumu hadi mwisho wa mchezo, na kuifanya Ndanda FC kuibuka na ushindi wa mabao 3-0.