Content removal request!


LIPULI FC 0-0 AZAM FC, (HIGHLIGHTS & INTERVIEWS) - 16/02/2018

Timu ya Azam FC imeshindwa kutamba mbele ya Wanapaluhengo, Lipuli FC ya Iringa kwa kulazimishwa suluhu katika mchezo wa raundi ya 19 ya Ligi Kuu Tanzania Bara. Wakicheza kwa kiwango kizuri uwanjani kwao Samora mkoani Iringa, Lipuli FC wameibana vilivyo Azam huku wakishindwa kutumia nafasi takriban tatu za wazi. Lipuli pia wamewazidi Azam umiliki wa mpira, wakimaliza mchezo wakiwa na umiliki wa asilimia 51 dhidi ya 49 za Azam.