Wagosi wa Kaya, Coastal Union wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara #NBCPremierLeague uliochezwa Desemba 5 kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga. Magoli ya Coastal Union yamefungwa na Vicent Abubakar dakika ya 2 pamoja na Aman Kyata dakika ya 76 huku Mbeya kwanza wakipata goli lao kupitia kwa William Edgar dakika ya 48