Mtibwa Sugar imepata ushindi wake wa kwanza leo kwa kuitandika Biashara United mabao 2-0 katika mchezo wa #NBCPremierLeague uliochezwa kwenye Dimba la Manungu, Turian Morogoro. Goli la kwanza kwa Mtibwa ilikuwa ni penati ya Nzigamasabo Styve huku goli la pili likiwekwa nyavuni na Said Ndemla.