Kikosi cha Simba SC,kimerejea Jijini Dar es salaam leo Februari 13,2024 kikitokea Jijini Mwanza baada ya kucheza michezo minne ya ligi kuu ya NBC katika Mikoa Mitatu,Februari 3 dhidi ya Mashujaa FC Kigoma,Februari 6 dhidi ya Tabora United, Tabora,Februari 9 dhidi ya Azam FC Mwanza na Februari 12 dhidi ya Geita Gold Mwanza. Kwenye Michezo hiyo Minne Simba SC imevuna Alama 10 kati ya 12,imemfunga Mashujaa FC 1-0,Ikamfunga Tabora United 4-0,Ikatoka Sare ya 1-1 na Azam FC na ikamfunga Geita Gold 1-0.