Mshambuliaji wa JKT Tanzania Ally Ahmed Shiboli ambaye aliingia kutokea benchi, alikumbana na rungu la mwamuzi Mbaraka Rashid baada ya kuonesha kitendo cha utovu wa nidhamu dhidi ya mwamuzi huyo. Tukio hilo limetokea dakika ya 88 wakati wachezaji wa JKT Tanzania wakidai kunyimwa penati baada ya mpira kumgonga mkononi beki wa Simba, Erasto Nyoni. Mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga umemalizika kwa Simba kupata ushindi wa mabao 2-0. Tazama ilivyokuwa.