Content removal request!


HIGHLIGHTS: MWADUI FC 1-0 MBAO FC (VPL - 30/04/2018)

Mwadui FC imepanda kutoka nafasi ya 12 hadi ya 9 kwenye msimamo baada ya kushinda bao 1-0 dhidi ya Mbao FC kwenye mechi ya Ligi Kuu soka Tanzania Bara iliyochezwa leo jioni Uwanja wa Mwadui Complex, Shinyanga. Bao pekee la Mwadui FC limefungwa dakika ya 29 na Charles Ilanfya aliyetumia vyema makosa ya golikipa Mussa Mohamed wa Mbao FC ambaye alipiga kimakosa mpira aliombabatiza mchezaji wa Mwadui FC, Salim Khamis. Hata hivyo, Mwadui walilazimika kucheza pungufu kwa dakika 38 za kipindi cha pili kutokana na golikipa wake, Anord Massawe kuoneshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kufuatia kuudaka mpira nje ya eneo lake akiwa mchezaji wa mwisho.