Content removal request!


SIMBA SC 8-1 COASTAL UNION: FULL HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (TPL - 08/05/2019)

Mnyama Simba SC amepata ushindi wa kishindi kwa kuipiga Coastal Union mabao 8-1 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara uliopigwa leo kwenye Dimba la Uhuru Jijini Dar es Salaam. Mchezo huo pia umeshuhudia zikipatikana hat-trick mbili kwa mara ya kwanza kwenye ligi hiyo msimu huu, moja ikitoka kwa Emmanuel Okwi akifunga dakika za 11, 20 na 47 huku nyingine ikipigwa na Meddie Kagere dakika za 67, 75 na 83. Mabao mengine yamefungwa Hassan Dilunga dakika ya 81 na Clatous Chama dakika ya 90+3 huku bao pekee la Coastal likifungwa na Raizin Haidh dakika ya 35. Ushindi huo sasa umeiweka Simba kileleni ikifikisha pointi 81 na kuishusha Yanga yenye pointi 80 huku Azam ikifuatia ikiwa na pointi 67.