Content removal request!


AFRICAN LYON 2-2 MBEYA CITY: HIGHLIGHTS & INTERVIEWS (18/05/2019)

Timu ya African Lyon ambayo tayari imeshuka daraja, imejiongezea pointi moja baada ya kutoka sare na Mbeya City, katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa kwenye Dimba la Uhuru Dar es Salaam. Lyon ndiyo waliotangulia kupata mabao yote mawili kupitia kwa Musht Bartoz dakika ya 21 na Awadhi Juma dakika ya 45+2 lakini Mbeya City walitumia dakika kumi za mwisho kusawazisha kupitia kwa Victor Hangaya dakika ya 82 na Mohamed Kapeta dakika ya 90+5. Matokeo hayo yameifanya Lyon kufikisha pointi 23 ikiwa mkiani mwa msimamo wa ligi huku Mbeya City ikifikisha pointi 47 na kupanda kwa nafasi moja hadi nafasi ya saba sawa na Ndanda SC ambayo imeshuka hadi nafasi ya nane.