Content removal request!


Tarehe na ratiba ya msimu mpya wa VPL 2018/19 vyatajwa, bodi ya ligi yaeleza vigezo

Bodi ya Ligi Tanzania Bara (TPLB) kupitia kwa Mtendaji wake Mkuu Boniface Wambura imetangaza msimu mpya wa ligi hiyo 2018/19 kuanza kutimua vumbi rasmi tarehe 22/08/2018 ukishirikisha timu 20. Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na bodi hiyo, watani wa jadi Simba na Yanga wamepangwa kukutana Septemba 30 mwaka huu ambapo Simba watakuwa wenyeji. Wambura amesema ratiba hiyo imezingatia ratiba ya michuano mingine ikiwemo michuano ya CAF itakayoanza mwezi Novemba mwaka huu, kalenda ya FIFA, Kombe la Mapinduzi pamoja na michuano ya CECAFA. Mechi ya ngao ya jamii kuashiria kuanza kwa msimu mpya wa ligi itapigwa Agosti 18, 2018 kwenye dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza, na itakuwa ni kati ya mabingwa wa ligi kuu msimu uliopita Simba SC dhidi ya Mtibwa Sugar ambao ni mabingwa wa Kombe la Shirikisho la Azam Sports. Tarehe 22/08/2018: Simba SC vs Tanzania Prisons, Ruvu Shooting vs Ndanda FC, Alliance vs Mbao FC, Coastal Union vs Lipuli FC, Singida United vs Biashara, Kagera Sugar vs Mwadui FC. Tarehe 23/08/2018: Stand United vs African Lyon, JKT Tanzania vs KMC, Mtibwa Sugar vs Yanga SC, Azam FC vs Mbeya City.