Afisa Mhamasishaji wa Yanga SC,Jimmy Kindoki ameeleza furaha yake baada ya kuteuliwa katika nafasi hiyo na kuwaomba Mashabiki na Wanachama wa Yanga SC kumpa Ushirikiano ili aweze kutimiza Majukumu yake ipasavyo. Pia Jimmy Kindoki hakusita kummwagia sifa Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Timu hiyo,Ally Kamwe kwa kusema anafanya kazi kubwa na nzuri. Vilevile amesema ana imani kubwa na Wachezaji wapya waliosajiliwa kwenye dirisha dogo.