“Kama klabu lazima tuoneshe kwamba kuna namna ambavyo hatujaridhishwa na kile ambacho kimetokea katika mchezo ule” sehemu ya maneno ya Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe akizungumzia hatua ambazo timu hiyo imepanga kuzichukua juu ya yale yaliyojiri katika dimba la Loftus kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Mamelodi Sundowns.