Simba SC imefuzu hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika #CAFCL kwa ushindi wa jumla wa mabao 4-1 baada ya leo kuichapa CD Primeiro de Agosto baoa 1-0 katika mchezo wa marudiano uliopigwa kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Goli pekee la Simba kwenye mchezo wa leo limetoka kwenye guu la Moses Phiri dakika ya 33.