Content removal request!


MAGOLI YOTE: SERENGETI BOYS 3-2 AUSTRALIA (UEFA ASSIST – 06/03/2019)

Timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 #SerengetiBoys imepata ushindi wake wa kwanza kwenye michuano maalum ya vijana yaliyoandaliwa na Chama cha Soka barani Ulaya (UEFA) yanayofahamika kwa jina la UEFA Assist. Katika michuano hiyo inayofanyika nchini Uturuki, Serengeti Boys imeitandika Australia mabao 3-2 baada ya kupoteza mchezo wake wa kwanza ilipofungwa na Guinea bao 1-0. Katika mchezo wa leo mabao ya Serengeti Boys yamefungwa na Edmund John, Edson Jeremiah Kelvin John huku mabao ya Australia yakifungwa na Ryan Tegue na Noah Botic. Azam TV kupitia channel ya #AzamSports2 inakuletea LIVE mechi zote zinazoihusu timu hii ya Tanzania. #UefaAssist #UefaCafAssist