Mtibwa Sugar imepata ushindi wake wa tatu msimu huu kwenye ligi baada ya kuichapa Mbeya Kwanza mabao 2-1 katika game iliyopigwa kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya. Mtibwa wametangulia kupitia kwa Mululi Mayanja , Mbeya wakachomoa kwa penati ya Habibu Kyombo lakini Mtibwa wakaongeza la pili kwa goli la Omary Sultan.