Katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliopigwa Novemba 23, 2018 kuna matukio kadhaa yaliyozua utata, kubwa likiwa ni bao alilofunga Meddie Kagere, lakini ikaamuliwa kuwa alikuwa off-side. Kwa mujibu wa Kipyenga cha Mwisho cha Azam Sports chini ya mwamuzi mstaasu Osman Kazi na Mkufunzi wa waamuzi Hemed Mteza, goli lile lilikuwa halali. Mbali na tukio hilo pia palikuwa na tukio lingine la Simba kunyimwa penati halali pamoja na matukio ya off-side. Yote haya ni kwenye kipindi cha Kipyenga cha Mwisho ambacho hukufikia kila Alhamis, saa 3;30 usiku Azam Sports 2.