Tazama jinsi timu ya Mbao FC ilivyobanwa mbavu na Lipuli FC katika dimba lake la CCM Kirumba Mwanza na kulazimishwa suluhu katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara (VPL) uliopigwa Ijumaa Aprili 6, 2018. Katika mchezo huo Mbao walitengeneza nafasi nyingi ndani ya eneo la 18 la Lipuli lakini walishindwa kufunga, huku pakitokea kituko cha gloves za kipa wa Lipuli kuibiwa na kutupwa nje ya uwanja tukio ambalo lilitokea dakika ya 45.