Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara, Simba SC imepata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Biashara United kwenye Dimba la Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Magoli yote matatu yamefungwa ndani ya dakika 20 za kwanza...akianza Pape Sakho dakika ya 9, Mzamiru Yassin dakika ya 14 na Clatous Chama dakika ya 18.