Timu ya JKT Tanzania imeamua kutumia Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga kama uwanja wake wa nyumbani kwa mechi za Ligi Kuu Tanzania zitakazohusisha Simba na Yanga. Uamuzi huo unatokana na uwanja wake wa nyumbani inaotumia sasa wa Meja Jenerali Isamuhyo ulioko Mbweni Dar es Salaam, kutokuwa na uwezo wa kuhimili wingi wa mashabiki wa timu hizo mbili vigogo nchini Tanzania.