DODOMA JIJI 1-0 NAMUNGO: Khamis Mcha 'Viali' amefunga goli pekee kwa mkwaju wa penati na kuipa Dodoma Jiji ushindi wa ...
DODOMA JIJI 1-0 NAMUNGO: Khamis Mcha 'Viali' amefunga goli pekee kwa mkwaju wa penati na kuipa Dodoma Jiji ushindi wa ...
namungofc #namungo #dodomajijifc #dodomajijifc #hengetv #live.
Tazama penati zote zilizopigwa kwenye mchezo wa fainali ya #crdbbankfederationcup kati ya Azam FC dhidi ya Yanga SC. Yanga imeshinda kwa jumla ya penati 6-5 na kutwaa kombe la Shirikisho la CRDB Benki kwa mara ya nne tangu lirejee mwaka 2015. Waliokosa penati kwa Yanga ni Stephane Aziz Ki, Joseph Guede na Ibrahim Abdullah Bacca. Waliokosa kwa Azam FC ni Iddy Nado, Gibril Sillah, Fuentes Mandoza na Lusajo Mwaikenda.
Tazama magoli yote matano yaliyofungwa kwenye mechi ya NBC Premier League kati ya Yanga SC dhidi ya Tanzania Prisons. Yanga imeshinda magoli 4-1. Stephane Aziz Ki amefunga hat trick na lingine limefungwa na Kennedy Musonda. Goli la Prisons limefungwa na Beno Ngasa
Joseph Guede, Maxi Nzengeli na Stephane Aziz Ki ndiyo waliotikisa nyavu za Tabora United na kuipa Yanga ushindi wa mabao 3-0 katika mchezo wa raundi ay 29 #NBCPremierLeague ukipigwa Benjamin Mkapa Stadium. Goli alilofunga Aziz Ki dakika ya 90 kwenye mchezo ni goli lake la 18 kwenye ligi msimu huu akizidi kukifukuzia kiatu cha ufungaji bora, akiwa na mechi moja mkononi.
Feisal Salum amefunga magoli mawili Azam FC ikiibugiza Kagera Sugar mabao 5-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC iliyopigwa leo kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi..... Magoli mengine kwenye mchezo huu yametoka kwa Gibril Sillah dakika ya 50’, Kipre Jr dakika ya 65' na Iddy Nado dakika ya 90, huku Feisal akifunga yake dakika ya 72 na 79.
Stephane Aziz Ki amefunga magoli mawili na kufikisha magoli 17 katika mbio za ufungaji bora, Yanga ikiibugiza Dodoma Jiji mabao 4-0 kwenye Dimba la Jamhuri, Dodoma. Ni mchezo wa #NBCPremierLeague uliofunguliwa na goli la Clement Mzize dakika ya 10 kabla ya Aziz kufunga mawili dakika ya 45+3 kwa penati na dakika ya 51, na kisha Maxi Nzengeli akafunga kazi kwa goli la nne dakika ya 78. Magoli yote manne haya hapa....
Simba SC imepata ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Geita Gold FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa leo Azam Complex, Chamazi. Geita walitangulia kwa goli la Geofrey Julius dakika ya 11, kabla ya Simba kusawazisha dakika ya 45 kwa penati ya Saidi Ntibazonkiza ambaye pia alifunga la pili dakika ya 72 kwa free-kick. Aliyekamilisha mabao mawili ya mwisho ni Ladaki Chasambi dakika ya 86 na 90..... Haya hapa magoli...
Goli pekee la Stephane Aziz ki limeipeleka Yanga fainali yake ya tano ya michuano ya #CRDBBankFederationCup ikishinda 1-0 dhidi ya Ihefu SC, mchezo wa nusu fainali uliopigwa Sheikh Amri Abeid Arusha. Yanga sasa itakutana na Azam FC katika mchezo wa fainali, Juni 02, 2024.
Goli pekee la Freddy Michael Koublan limeipa Simba pointi tatu muhimu, wakiichapa Dodoma Jiji 1-0 kwenye Dimba la Jamhuri, Dodoma. Hii ni #NBCPremierLeague