Afisa Mhamasishaji wa Yanga SC,Jimmy Kindoki ameeleza furaha yake baada ya kuteuliwa katika nafasi hiyo na kuwaomba Mashabiki na Wanachama wa Yanga SC kumpa Ushirikiano ili aweze kutimiza Majukumu yake ipasavyo. Pia Jimmy Kindoki hakusita kummwagia sifa Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Timu hiyo,Ally Kamwe kwa kusema anafanya kazi kubwa na nzuri. Vilevile amesema ana imani kubwa na Wachezaji wapya waliosajiliwa kwenye dirisha dogo.
Leo Mei 13,2024 Mtibwa Sugar inashuka Dimba la Manungu Turiani kumenyana na Yanga SC katika mchezo wa ligi kuu ya NBC,,Saa 10 jioni.
Leo May 08,2024 katika uwanja wa Azam complex kutachezwa mchezo mmoja wa NBC PREMIER LEAGUE ambao utazikutanisha Yanga SC dhidi ya Kagera Sugar