KAGERA SUGAR YALALA NA VIATU, YAPIGWA 2-0 NA RUVU SHOOTING by @Siajabu Omary - Post Details

KAGERA SUGAR YALALA NA VIATU, YAPIGWA 2-0 NA RUVU SHOOTING

KAGERA SUGAR YALALA NA VIATU, YAPIGWA 2-0 NA RUVU SHOOTING Na Omary Mngindo, Mlandizi Pwani Tanzania- Feb 8 TIMU ya soka ya Ruvu Shooting ya Mlandizi Kibaha Pwani Tanzania Alhamisi ya Feb 8 imeendelea kuutumia vema uwanja wake wa nyumbani baada ya kuilaza na "VIATU" Kagera Sugar ya mkoani Kagera kwa mabao 2-0. Mchezo huo uliokuwa mkali na kuvutia kwa muda wote, washindi walioutumia uwanja wa nyumbani, ilibidi wasubiri mpaka kipindi cha pili kujipatia mabao hayo yaliyofungwa na Mcha Khamis kwa njia ya penati, wakati bao la pili likiwekwa kambani na Alinanuswe Martin akimalizia krosi kutoka magharibi ya uwanja. Mpaka dakika 90 za mwamuzi wa mchezo huo, Shooting imejipatia ushindi wa pili mfululizo katika uwanja wake wa nyumbani baada ya kuibuka na idadi kama hiyo dhidi ya Mbao FC ya jijini Mwanza uliochezwa majuma hivi karibuni. MWISHO.R

Similar Posts!

MASHABIKI RUVU SHOOTING WAKISHANGILIA USHINDI WA KWANZA DHIDI YA NDANDA FC
MASHABIKI RUVU SHOOTING WAKISHANGILIA USHINDI WA KWANZA DHIDI YA NDANDA FC

MASHABIKI RUVU SHOOTING WAKISHANGILIA USHINDI WA KWANZA DHIDI YA NDANDA FC Na Omary Mngindo, Mlandizi, Kibaha Vijijini, Pwani, Tanzania- Nov 18 BAO la pekee la timu ya soka ya Ruvu Shooting dhidi ya Ndanda Fc ya Mtwara lililofungwa na Abdulhaman Mussa kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) limepokelewa kwa shangwe, furaha na vifijo kutoka kwa mamia ya mashabiki wa timu hiyo wengi wao wakiwa vijana waliojiunga na Kikosi cha JKT kwa ajli ya mafunzo. Bao hilo lililofungwa kwa mkwaju wa penati na nyota huyo aliyekuwa mfungaji bora katika Ligi ya msimu uliopita akifungana na kiungo aliyekuwa anakitumikia kikosi cha Yanga Simon Msuva, limeiwezesha timu hiyo kupata ushindi wa kwanza kwenye kinyang'anyiro hicho tangu kuanza kwa ligi ya msimu huu. MWISHO.