KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imefanya kweli baada ya kuidungua Mwadui bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) uliomalizika Uwanja wa Azam Complex usiku huu. Ushindi huo unaifanya Azam FC kusogea hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi ikifikisha jumla ya pointi 41 na kuishusha Yanga yenye mechi mbili mkononi hadi nafasi ya nne ikibakiwa na pointi zao 40 huku Simba ikiwa kileleni kwa pointi 46. Bao pekee la Azam FC limewekwa kimiani na mshambuliaji Yahya Zayd, dakika ya tano akitumia uzembe wa kipa wa Mwadui, Anold Massawe, aliyepiga mpira vibaya na kumpasia mguuni mfungaji wakati akiwa kwenye harakati za kuupiga mbele mpira aliorudishiwa na beki wake, Idd Mfaume.
KLABU ya Azam FC imeanza vema kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) msimu 2020/2021 baada ya kuichapa Polisi Tanzania bao 1-0 kwenye mchezo wa kwanza. Bao pekee la Azam FC limewekwa kambani na mshambuliaji Obrey Chirwa, dakika ya 44 akiunganisha krosi safi ya mshambuliaji mpya, Prince Dube. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora #SARAFU #AzamUkwaju #AzamUbuyu #AzamStrawberry #UhaiDrinkingWater
#ObreyChirwa #IddNado #AzamFC #SingidaUnited Azam FC imeandika rekodi ya kwanza baada ya kupata ushindi mnono wa kihistoria kwenye mechi za mashindano, ikiichapa Singida United mabao 7-0, ukiwa ni mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL). Mabao ya Azam FC yalifungwa na Obrey Chirwa akifunga manne, Idd Seleman 'Nado', akifunga mawili huku jingine wakijifunga wenyewe Singida United. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora
KLABU ya Azam FC imeendelea pale ilipoishia kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) baada ya kuichapa Mbaoa mabao 2-0 jana Jumapili usiku. Mabao ya Azam FC yalifungwa na washambuliaji Richard Djodi na Shaaban Chilunda. #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora
HIGHLIGHTS | AZAM FC 2-2 JKT TANZANIA | 2019/2020 SEASON
Kikosi cha Azam FC kimeendeleza wimbi la ushindi ugenini kwenye mechi za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kwa kupata ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Alliance. Mabao matatu ya Obrey Chirwa (hat-trick) na mawili ya Shaaban Chilunda, yalitosha kabisa kuihakikishia ushindi mwingine Azam FC mkoani Mwanza, ikifanikiwa kuvuna pointi zote sita. #ObreyChirwa #ShaabanChilunda #WeAreAzamFC #TimuBoraBidhaaBora