KIKOSI cha timu ya vijana ya Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Azam FC U-20, kimeondoka jijini Dar es Salaam leo Alhamisi asubuhi kuelekea mkoani Dodoma tayari kushiriki michuano ya Ligi ya Vijana (Uhai Cup U-20) kwa timu za vijana za klabu zinazoshiriki Ligi Kuu.