Simba Full Mkoko Mbeya |Pape Sakho, Chama,Morrison| Mazoezi ya Mwisho na Kikosi Kilivyoingia Uwanjani Simba Sports Club, wawakilishi wa nchi katika mashindano ya kimataifa wako jijini Mbeya tayari kwa maandalizi ya mchezo wa NBC Premier League dhidi ya Mbeya City. Na ikumbukwe tu Simba wameenda kuwakabili Mbeya City wakiwa na kiungo wao machachari waliyemsajili tena katika dirisha dogo, si mwingine bali ni Mwamba wa Lusaka, Clatous Chota Chama. Sasa kupitia mitandao ya kijamii ya Simba Sports Club, mabingwa hao watetezi wameonekana wakiwa mazoezini full mkoko yaani wachezaji wao wote waliowasajili akiwemo Chama. Haya ni mazoezi ya mwisho kwa Simba kabla ya kuwakabili Mbeya City katika mechi muhimu kwa Simba kutetea ubingwa wao wa Ligi Kuu. Na tukujuze tu kwamba baada ya Chama aliyekuwa akivaa jezi namba 17 kuondoka Simba, jezi yake alikabidhiwa Pape Osman Sakho lakin mazoezini alionekana Sakho akiwa amevaa jezi namba 10 iliyokiwa ikivaliwa na Ibrahim Ajib aliyemtikia Simba na hii inamaanisha Chama amerudishiea jezi yake namba 17. Mechi ya leo ya Simba dhidi ya Mbeya City ni muhimu kwako katika kutetea ubingwa wao na wanaingia uwanja wa Sokoine wakiwa na kumbukumbu ya ushindi katika mchezo wao wa mwisho wa ligi. Je, Mbeya City atakubali kupoteza mchezo huu akiwa nyumbani? vipi wanasimbazi wataendeleza ubabe wao na kupunguza gap la points dhidi ya watani wao Yanga!? Dakika 90 ndio zitatoa majibu yote haya. Lakin kwako mtazamaji usisite kuacha maoni yako kuhusu hii mechi muhimu ya Mbeya City dhidi ya Simba.