Content removal request!


VPL Round 10: Njombe Mji 0-1 Azam FC - November 19, 2017

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, imeendeleza wimbi la ushindi kwenye Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) baada ya kuichapa Njombe Mji bao 1-0, mchezo uliofanyika Uwanja wa Sabasaba, mkoani Njombe jioni ya leo. Alikuwa ni Nahodha Msaidizi wa Azam FC, Agrey Moris aliyekuwa nahodha wa mchezo wa leo, akiihakikishia ushindi timu hiyo kwa bao safi la mkwaju wa penalti dakika ya 60 baada ya Enock Atta kufanyiwa madhambi kwenye eneo la hatari.