UGANDA VS TANZANIA 0 -0 Kikosi cha Taifa Stars, kimelazimishwa sare ya bila kufungana kikiwa ugenini dhidi ya wenyeji wake Uganda. Mechi hiyo ya kuwania kufuzu Afcon imepigwa kwenye Uwanja wa Namboole jijini Kampala na Stars iliyokuwa ikiongozwa na nahodha Mbwana Samatta imeonyesha soka safi na kuwapa wakati mgumu Uganda. Stars ilifanya mashambulizi mengi zaidi langoni mwa Uganda, hasa katika kipindi cha pili, hali iliyowalazimisha walinzi wa Uganda kufanya faulo nyingi zaidi. Kipindi cha kwanza ilionekana Uganda wakiwa na nafasi nyingi ambazo hawakuzitumia huku mvua kubwa iliyonyesha dakika chache kabla ya mechi ikiwa imechangia kuvurugika kwa uwanja huo. Install GlobalPublishersApp Android: http://bit.ly/2AAQe1d iOS: http://apple.co/2Assf4M Subscribe http://ww.youtube.com/c/uwazi FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublis... TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari Visit https://globalpublishers.co.tz/, Suazi1 http://www.youtube.com/c/uwazi1 WEBSITE: https://globalpublishers.co.tz/ FACEBOOK: https://www.facebook.com/Globalpublis... TWITTER: https://twitter.com/GlobalHabari INSTAGRAM: https://www.instagram.com/globalpubli..SSI