SIMBA Vs SEVIILA - KIKOSI cha SIMBA Kilivyowasili UWANJANI Taifa! LEO ni siku nzuri ya burudani hasa kwa wapenda mpira hasa baada ya kutua nchini kwa kikosi maarufu nchini Hispania na barani Ulaya cha Sevilla. Sevilla wako nchini kuivaa Simba na ziara yao imedhaminiwa na kampuni ya michezo ya kubeti ya SportPesa ambayo hii ni mara ya pili inaleta timu kubwa na maarufu baada ya Everton FC. Watanzania wapenda soka watarajie burudani ya soka la kuvutia na Simba watalazimika kujipanga na vizuri wakijiachia ili kucheza soka la uhakika linaloweza kuwafanya Sevilla kujiuliza. Hata hivyo, ubora wa Sevilla uko juu, hawa ni mabingwa mara tano Europa League lakini hii haitawazuia wao kutofungwa kama Simba watajipanga vizuri. Hata hivyo, kocha mkuu wa Sevilla ni mmoja wa makocha watundu, anajiamini hakika anatumia mfumo mmoja anaoubadilika mara kwa mara. Kocha Mkuu Joaquín Caparrós aliwahi kuifundisha Sevilla mwaka 2000 hadi 2005 kabla ya kujiunga na Deportivo la Coruna ya Kaskazini Magharibi mwa Hispania. Lakini baadaye alizifundisha timu kadhaa katika La Liga kama Athletic Bilbao, Mallorca, Granada na Osasuna kabla ya kuhamia nchini Qatar na kuanza kuinoa A Ahli kwa mwaka mmoja kabla ya kurejea tena Hispania na kuwa kocha wa muda wa Sevilla ambayo baadaye alikabidhiwa mikoba. #SIMBAVsSEVILLA Https://www.youtube.com/watch?v=N1X-f... Watch More Videos here: https://goo.gl/GvVdZw Watch More Videos here: https://goo.gl/ae33fL Website: www.globalpublishers.co.tz FaceBook: www.facebook.com/globalpublishers Instagram: www.instagram.com/globalpublishers Twitter: www.twitter.com/GlobalHabari Install Global App: ANDROID: https://goo.gl/QvT6RV Install Global App: iOS: https://goo.gl/2jDyho