Mabingwa wa ligi ya KPL, Tusker watakuwa na kibarua kigumu hapo kesho watakapo menyana na Gor Mahia katika mechi ya ligi ya premia nchini. Mechi hiyo itang'oa nanga mwendo wa saa moja katika uga wa nyayo. mechi hiyo ni muimu kwa timu hizo mbili. Tusker wako katika nafasi ya saba na alama saba kutokana na mechi nne ilhali Gor Mahia wamejipata katika nafasi ya 13 na alama tatu kutoka mechi tatu. Klabu ya AFC Leopards watakuwa wakitazama mechi hiyo kwa maakini sana kwani maasimu hao wamepangiwa kukutana siku ya jumapili katika mechi yenye msisimko. Kwa sasa, leopards wanaongoza jedwali wakiwa na alama 13 na matokeo ya mechi ya kesho haiwatishi. Tusker nao watakuwa wakicheza kwa uangalifu kwani wanakibarua siku ya jumamosi dhidi ya karuturi katika uwanja wa Nyayo. Sofapaka ambao wako katika nafasi ya pili, alama mbili nyuma ya AFC Leopards wamepangiwa kucheza Western Stima siku ya jumapili. Western Stima watatoana kijasho na Ranger Jumatano kuanzia saa tisa ugani Nyayo