Content removal request!


INASIKITISHA SAKATA LA MCHEZAJI KUKATWA MGUU/POLISI TANZANIA WASEMA KUHUSU KUMTELEKEZA MCHEZAJI WAO

GERALD ANAHITAJI MSAADA. Kijana Gerard Mathias Mdamu anateseka kitandani pale MOI Nadhani huu sio wakati wa kulaumiana na kuanza kunyoosheana vidole kuonyesha nani anakosea na nani yuko sahihi Jeshi la Polisi linajitahidi kumsaidia Mdamu na familia kwa nafasi yake inamsaidia Mdamu. Timu zilizo chini ya taasisi za serikali, taratibu zake hasa katika suala la fedha huwa zina mlolongo mrefu lakini sio kwamba Polisi Tanzania haitaki kumhudumia Mdamu. Kwa wakati huu nadhani ni jambo jema tukasaidia kuokoa miguu ya Mdamu kisha baada ya hapo tukarudi katika kulaumiana. Tumsaidie kijana na Mtanzania mwenzetu kwa chochote kile ambacho tumejaliwa ili kunusuru asikatwe miguu. Hii inaweza kuwa sadaka ambayo inaweza kutusaidia leo hapa duniani na kesho mbele ya muumba Haya shime Watanzania wenzangu Tuma mchango wako kupitia kwa namba hii ya simu 0714716843. Jina ni BENEDICTOR MDAMU Kaka yake Mdamu. ✍️@charlesabel24. @KitengeUpdates.