Mbao FC imeshindwa kutumia vyema uwanja wake wa nyumbani (CCM Kirumba) baada ya April 6 kulazimishana suluhu na Lipuli katika mchezo wa Ligi Kuu. Katika mechi hiyo wakati wa mapumziko, palizuka vurugu kwa makomandoo wa timu zote mbili na kusaidiwa na Askari Polisi waliofika kutuliza ghasia hizo.