MAZISHI ya JOTA YAACHA SIMANZI KWAO - RONALDO AACHA MASWALI KUSHINDWA KUFIKA MAZIKONI... Mazishi ya mshambuliaji wa Liverpool, Diogo Jota, yamefanyika leo katika mji wake wa kuzaliwa wa Gondomar, nchini Ureno, ambapo mamia ya waombolezaji, wakiwemo familia na marafiki wa karibu, walikusanyika kumuaga pamoja na kaka yake, André Silva, waliofariki katika ajali mbaya ya gari siku ya Alhamisi, Julai 3, 2025. Mke wa Jota, Rute Cardoso, mwenye umri wa miaka 28, alionekana akitokwa na machozi huku akitembea taratibu nyuma ya jeneza la mumewe, akiwa amevaa mavazi meupe na kushikilia waridi la rangi ya krimu. Jota ameacha watoto watatu — wavulana wawili na binti mmoja. Baadhi ya waombolezaji walionekana wakisaidiwa na wenzao kutokana na mshtuko na majonzi makubwa yaliyowakumba. Majeneza ya Diogo Jota na kaka yake André yalipelekwa kwa huzuni kubwa hadi ndani ya kanisa lililoko Gondomar. Ni watu wa familia na marafiki wa karibu pekee walioruhusiwa kuingia ndani ya kanisa hilo, lakini misa ya mazishi ilipeperushwa moja kwa moja kupitia spika kwa maelfu ya waombolezaji waliokuwa wamejipanga nje kuonyesha heshima zao za mwisho. ============================================================ ⚫️ JE, NA WEWE UNA HABARI? ⚫️ WASILIANA NA GLOBAL TV ONLINE: ( +255 739 750910), ( +255 783453136) ⚫️ Email: globaltvonlinenews@gmail.com ⚫️ OUR PLAYLISTS: ⚫️ MICHEZO na BURUDANI: https://www.youtube.com/playlist?list=PL22mc2rU91vD-h-a328gR3qltQXYWVQiO ⚫️ HISTORIA ZA VIONGOZI ZA KUSISIMUA: http://bit.ly/mikasa_ya_kusisimua ⚫️ GLOBAL RADIO TV: http://bit.ly/255globalradio ⚫️ EXCLUSIVE INTERVIEW: http://bit.ly/exclusive_interviews ⚫️ SIKILIZA + 255 GLOBAL RADIO LIVE: http://ndstream.net/globalradio/ ⚫️ Kwa UPDATES zote, Download GLOBAL APP: ⚫️ ANDROID:http://bit.ly/38Lluc8 ⚫️ iOS:https://apple.co/38HjiCx