Content removal request!


SASA YANGA SC KUVAANA NA ZESCO UNITED KOMBE LA SHIRIKISHO BARANI AFRICA.

Baada ya kufanikiwa kuitoa Township Rollers kwenye hatua ya awali Klabu Bingwa Afrika, Yanga SC sasa katika raundi ya kwanza ya michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika watacheza dhidi ya Zesco United ya Zambia. Ikumbukwe Zesco United wamefika hatua hiyo baada ya ushindi wa jumla ya goli 3-0 dhidi ya Green Mamba ya Eswatini. Yanga SC wataanzia nyumbani Tanzania na kumalizia ugenini nchini Zambia, mechi ya kwanza itapigwa kati ya Septemba 13-15  marudiano kuchezwa kati ya  Septemba 27-29 mwaka huu. Baada ya hapo, mshindi wa hatua hii atafuzu katika hatua ya makundi ya michuano hiyo ya Afrika.