Tathmini yakinifu kutoka kwa Ghalib Mzinga Mchambuzi na Mtangazaji wa soka kutoka Azam Media LTD, kuelekea mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Wydad Athletic Club dhidi ya Simba SC. Mzinga anaamini utakuwa ni mchezo mgumu licha ya Wydad kuonekana hajaanza vyema katika Michezo yake ya awali.
Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga Ally Kamwe, amezungumza na Mpenja TV na kuelezea Mipango ya Timu yake kuelekea katika Mchezo wa CRDB Federation Cup Dhidi ya Dhidi ya Tabora United Mchezo ambao utachezwa May 1,2024 katika uwanja wa Azam Complex Pia Ally Kamwe amegusia kuhusu tetesi za Mchezaji wao Pacome Zouzoua na kuweka wazi kinachoendelea mpaka sasa.