Kikosi cha Simba SC kimewasili Jijini Dar Es Salaam Alasiri ya leo Machi 1, 2022 kikitokea Nchini Morocco ambako kilipoteza mchezo wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya wenyeji RS Berkane kikifungwa 2-0. Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, ametamba kwamba sasa RS Berkane wajiandae kuvuta pumzi ya moto kwa Benjamin Mkapa Machi 13, mwaka huu. #SimbaSC #AhmedAlly #MpenjaTV