Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo wa NBC Premier League kati ya Simba SC dhidi ya Mashujaa FC. Simba imeshinda kwa jumla ya magoli 2-1. Magoli ya Simba yamefungwa na Leonel Ateba kwa mikwaju ya penati. Goli la Mashujaa limefungwa na Jafary Kibaya
YANGA DAY: Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mchezo wa kirafiki kati ya Yanga SC dhidi ya Aigles du Congo. Goli la Yanga limefungwa na Peter Shalulile na magoli ya Aigles du Congo yamefungwa na Talasy Tonny. FT: Yanga SC 1-2 Aigles du Congo #YangaDay #YangaSC #MwakaniTena #Wananchi #MechiYaKirafiki #YangaSC #AiglesduCongo
SIMBA DAY: Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mechi ya kirafiki kati ya Simba SC dhidi ya Kenya Police Goli limefungwa na Elvis Rupia. FT: Simba SC 0-1 Police Kenya #SimbaDay #SimbaSC #Miaka90 #MechiYaKirafiki #SimbaSC #KenyaPolice
SIMBA DAY: Eba hii kali…Semaji Ahmed Ally aingia na simba wawili wa porini…Kila mtu abaki mdomo wazi. Neno moja tu kwa semaji Ni shamrashamra za #SimbaDay #SimbaDay #SimbaSC #Miaka90
Fuatilia uchambuzi na mengi yaliyojiri dimbani baada ya mchezo wa Ligi Kuu ya NBC kati ya Simba vs Yanga uliopigwa kwenye Uwanja wa Meja Jenerali Isamuhyo, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya mabao 2-2. Ndani ya studio Patrick Nyembera akiwa na wachambuzi Abissay Stephen na Godlisten Maro. Matangazo yako LIVE #AzamSports1HD lakini unaweza pia kuitazama kupitia katika #AzamTVMaxApp ►INSTAGRAM: https://www.instagram.com/azamtvtz/ ►INSTAGRAM: https://www.instagram.com/azamsports2/ ►TWITTER: https://twitter.com/azamtvtz ►FACEBOOK: http://www.facebook.com/azamtvtz ►WEBSITE: http://www.azamtv.co.tz
Simba SC imekabwa koo na kulazimishwa suluhu na Mogadishu City Club ya Somalia, katika mchezo wake wa kwanza wa Kombe la Kagame 2026, ukipigwa kwenye Dimba la Kigali, Rwanga. Kwenye mchezo huu Simba imewatumia baadhi ay nyota wake wapya akiwemo Ibrahim Doumbia , Cooper, Kelvin Nashon na wengine. Tazama highlights.
KAMWE AKWEPA KUMZUNGUMZIA AZIZ KI: Meneja Habari na Mawasiliano wa Yanga SC, Ally Kamwe anasema hakuna timu Afrika ambayo haipendi kuwa na mchezaji mwenye daraja la Stephane Aziz Ki, japo amekwepa kuzungumzia kwa undani tetesi zinazomhusisha kurejea mitaa ya Jangwani. Kamwe pia amesema kuna mchezaji walimpandisha thamani makusudi ili watu walipe hela nyingi. Kamwe amesema hayo leo kwenye mahojiano maalumu kupitia kipndi cha U-LIVE cha @ufmradiotz #YangaSC #Kamwe #UFM #ULIVE