WENYEJI, Mtibwa Sugar wameambulia sare dhidi ya Mabingwa watetezi, Simba SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Mangunu Complex, Turiani mkoani Morogoro. Kwa Matokeo hayo Mtibwa Sugar inafikisha pointi 12 baada ya michezo 13 na kusogea nafasi ya 13, wakati Simba SC inafikisha pointi 25 baada ya michezo 12, ingawa inabaki nafasi ya pili, ikizidiwa pointi saba na watani wao wa jadi Young Africans SC baada ya timu zote kucheza mechi 12. PLEASE DON'T FORGET TO SUBSCRIBE