Mpenja TV's user profile page. Match highlights, posts and more on site!“” Report User |
Mpenja Tv tumezungumza na Mchambuzi wa Soka kutoka Azam Media Limited Ramadhan Mbwaduke kuhusu takwimu za Kocha Roberto Oliveira "Robertinho" ndani ya Klabu ya Simba tangu alivyoanza kuifundisha na nini anakiona kwa Simba Msimu ujao wa 2023/2024. Pia amesema licha ya Simba SC kumaliza ligi wakiwa nafasi ya pili bado kocha Robertinho ana Takwimu Bora ukilinganisha na kocha Nasreddine Nabi ambaye ametwaa Ubingwa wa Makombe yote makubwa ngazi ya Klabu Nchini,Fainali Kombe la Shirikisho Afrika.
Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ tayari ipo kambini kujiandaa na mechi ya Kundi F dhidi ya Niger kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika ‘Afcon 2023’ itakayopigwa Jumapili kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, huku timu hiyo ikihitaji ushindi kwa lengo la kujiweka pazuri kwenda Ivory Coast.
USM Alger walishinda kwenye Dimba la Benjamin Mkapa na Yanga wameenda kushinda Kwenye Dimba la July 5, kila mmoja ameshindwa kwenye Ardhi ya Ugenini lakini Kombe limeenda kwa USM Alger. Hii ni tathmini ya Gharib Mzinga 'KILWA FINEST' Kuhusu Mchezo wa Pili wa Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika. Mzinga ameeleza kuhusu mipango ya Timu za Algeria kuhakikisha wanakuza vipaji na kufikia Nchi ya ahadi yenye Mafanikio ya Kisoka. Aidha ameeleza kuwa USM Alger hawajabadilika bali Yanga ndio walibadilika.
Leo Tarehe 29 Mei,Mpenja Tv tumefanya Mahojiano na Meneja Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba Sc Ahmed Ally na kuweka wazi Mwenendo wa Timu hiyo wakati huu ambao Ligi Kuu imesimama wakiwa wamebakiza Mechi Mbili Msimu kwisha.
Mchambuzi wa Soka kutoka Azam Media LTD ,Gharib Mzinga amewachambua kiundani wapinzani wa Yanga SC, USM Alger ambao watacheza nao Mchezo wa Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika,Jumapili hii Mei 28 2023,Katika Dimba la Benjamin Mkapa.
Mara ya kwanza Timu kutoka Tanzania imetinga hatua ya Fainali Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kumchabanga Marumo Gallants Goli 2 kwa 1 Nyumbani kwake. Mmoja wa Mashuhuda wa Rekodi hiyo ni Mwamba wa Umalila Baraka Adson Mpenja ambae ametoa maoni yake juu ya Rekodi hiyo na Ubora wa Kikosi cha Yanga. Aidha amenyoosha Mikono kwa Nyota Fiston Mayele juu ya Ubora alionao akiwa Kiwanjani, Goli moja na Pasi moja ya mwisho. Mpenja amekiri kuwa Msimu huu Yanga anakuwa Bingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika, na Kizazi hiki ndio Kizazi Bora cha Yanga tangu kuanzishwa kwake kwa mujibu wa Rekodi.
Leo Tarehe 10/05/2023 kwenye Dimba la Benjamin Mkapa kunapigwa Mchezo wa kwanza wa hatua ya Nusu Fainali Kombe la Shirikisho Afrika Yanga dhidi ya Marumo Gallants kutoka Afrika Kusini. Mchezo wa pili ulipigwa Afrika Kusini Tarehe 17/05/2023. Leo inatafutwa Tiketi ya kwenda hatua ya Nusu Fainali hapa Uwanja wa Benjamin Mkapa. Mpenja Tv tutakuletea matukio yote kabla na baada ya Mchezo huu kufika Tamati
Leo Mei 3 2023, katika Dimba la Majaliwa Ruangwa Mkoani Lindi inapigwa Mbungi ya Ligi kuu ya NBC kati ya Wauaji wa kusini,Namungo FC na Mnyama,Simba SC,Saa Moja Jioni . Mpenja TV tunakuletea Taarifa zote kabla na baada ya Mbungi hiyo
Mpenja TV ipo Jijini Dodoma kukuletea Updates zote za Mchezo wa ligi kuu kati ya Dodoma Jiji FC na Simba SC. Fungua video ...
Mpenja TV ipo Jijini Dodoma kukuletea Updates zote za Mchezo wa ligi kuu kati ya Dodoma Jiji FC na Simba SC. Fungua video ...
Mpenja TV ipo Jijini Dodoma kukuletea Updates zote za Mchezo wa ligi kuu kati ya Dodoma Jiji FC na Simba SC. Fungua video ...
Mpenja TV ipo Jijini Dodoma kukuletea Updates zote za Mchezo wa ligi kuu kati ya Dodoma Jiji FC na Simba SC. Fungua video ...
Mpenja TV ipo Jijini Dodoma kukuletea Updates zote za Mchezo wa ligi kuu kati ya Dodoma Jiji FC na Simba SC. Fungua video ...
Mpenja TV ipo Jijini Dodoma kukuletea Updates zote za Mchezo wa ligi kuu kati ya Dodoma Jiji FC na Simba SC. Fungua video ...
Mpenja TV ipo Jijini Dodoma kukuletea Updates zote za Mchezo wa ligi kuu kati ya Dodoma Jiji FC na Simba SC. Fungua video ...
Mpenja TV ipo Jijini Dodoma kukuletea Updates zote za Mchezo wa ligi kuu kati ya Dodoma Jiji FC na Simba SC. Fungua video ...