KidaniStars's user profile page. Match highlights, posts and more on site!

“”

 Report User

Highlights

Taifa Stars Yafuzu Kucheza Fainali za CHAN 2020, Sudan 1-2 Tanzania (Agg: 2-2):
Taifa Stars Yafuzu Kucheza Fainali za CHAN 2020, Sudan 1-2 Tanzania (Agg: 2-2):

Tanzania yafuzu fainali za CHAN mwaka 2020 kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2009. Ni baada ya kushinda 2-1 dhidi ya Sudan na kufuzu kwa faida ya goli la ugenini. Magoli ya Tanzania kwenye mchezo wa leo yamefungwa na Erasto Nyoni dakika ya 49 na Ditram Nchimbi dakika ya 78. FT | Sudan 1-2 Tanzania (Agg: 2-2) Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/Kidanistars



SIMBA Yaichapa 3-0 KAGERA Sugar,  Yaongoza Ligi, Kagere Atupia 2
SIMBA Yaichapa 3-0 KAGERA Sugar, Yaongoza Ligi, Kagere Atupia 2

Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars SIMBA SC imeanza mapema utawala katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa 3-0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba Septemba 26, 2019. Kikosi cha Kagera Sugar kilikuwa; Said Kipao, Mwaita Gereza, David Luhende, Hassan Isihaka, Erick Kyaruzi/Juma Nyoso dk46, Zawadi Mauya, Awesu Awesu, Ally Ramadhani, Evarigestus Mjwahuki, Abdallah Seseme na Yussuf Mhilu/Peter Mwalyanzi dk50. Simba SC; Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Tairone Santos, Serge Wawa, Gerson Fraga ‘Viera’, Deo Kanda/Miraj Athuman dk62, Muzamil Yassin, Meddie Kagere/Wilker Da Silva dk87, Sharaf Eldin Shiboub na Ibrahim Ajibu/Hassan Dilunga dk71. Mechi nyingine ya Ligi Kuu, Lipuli FC wamelazimishwa sare ya 2-2 na Mbeya City Uwanja wa Samora mjini Iringa. Mabao ya Lipuli FC yamefungwa Issa Rashid dakika ya 15 na Paul Nonga dakika ya 77, wakati ya Mbeya City yamefungwa na George Chota dakika ya 47 na Ibrahim Mwakamole dakika ya 86. Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/Kidanistars



SIMBA Yavunja Rekodi Ya KAGERA Sugar, Zipo Hapa
SIMBA Yavunja Rekodi Ya KAGERA Sugar, Zipo Hapa

Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/Kidanistars



SIMBA SC 2-1 MTIBWA SUGAR, Simba Walivyotua Taifa Kibabe
SIMBA SC 2-1 MTIBWA SUGAR, Simba Walivyotua Taifa Kibabe

Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars FULL TIME: SIMBA SC 2-1 MTIBWA SUGAR Dak ya 90+3, kadinya njano inakwenda kwa Salum Kanoni, dakika za jioni kabisa. Dakika zimeongezwa tatu kumaliza mpira, zimesalia mbili sasa. Dak ya 90, Jonas Mkude anaingia kuchukua nafasi ya Shiboub Dak ya 81, Imepigwa faulo ile kwake Kahata inamkuta na anajaribu kumalizia lakini mpira unamzidi kasi, golikiki. Dak ya 81, Mtibwa wanacheza faulo, inapigwa kuelekezwa langoni kwao, nafasi ya Simba kupata bao la tatu. Dak ya 79, Kahata anaingia kuchukua nafasi ya Chama. Dak ya 77, Kona nyingine kwa Simba, ni baada ya Kapombe kubabatizana na Kapombe. Inapigwa lakini inakuwa golikiki. Dak ya 74, Simba wanaanza tena upya, Yassin kwake Athuman, piga kwake Kado anadaka mpira. Dak 68, Mirajiiiiii, anaifungia Simba bao la pili kwa shuti kali akitoka kupokea pasi nzuri kutoka kwa Shiboub Dak ya 67, Mtibwa wanaonesha jitihada za kulinda zaidi eneo lao na wakifanya mashambulizi ya kushtukiza kwa Simba. Dak ya 63, Simba wamefanya shambulizi la kutisha langoni mwa Mtibwa lakini mawasiliano yamekuwa si mazuri na Mtibwa wanaokoa. Dak ya 62, Miraji Athuman anaingia kuchukua nafasi ya Hassan Dilunga. Dak ya 60, Simba wameanza tena, Chama anachukua, anampasia Nyoni, wanajribu kupenya ngome ya Mtibwa, kwake Kagere lakini Mtibwa wanawadhibiti. Dak ya 57, Tayari Kado ameshasimama na mpira umeshaanza, Simba wanaanza kwa kupasiana vema langoni mwa Mtibwa, unamkuta kwake Chama, anapiga shuti ambalo linapaa nje ya lango. Dak ya 55, Mpira umesimama, Kado ameumia, Kahata naye anaonekana kama anataka kuchukua nafasi ya mtu. Dak ya 52, Kado anaokoa nafasi nyingine kutoka kwa Yassin aliyepata nafasi ya kufunga, kama angekuwa dhaifu angeshafungwa zaidi ya bao mbili. Dak ya 52, Kagere anaotea, anaonekana kulalamika kwa kuonesha ana njaa ya kufunga. Dak ya 49, Aishi Manula anaanzisha upya mashambulizi, ni kipindi cha pili sasa. MAPUMZIKO: SIMBA SC 1-1 MTIBWA SUGAR Dak ya 47, Chama amepiga lakini inakwenda nje. Dak ya 46, Humud anapewa kadi ya njano baada ya kucheza madhambi, ni ya kwanza ndani ya dakika 45 za kwanza, ni faulo. Dak ya 44, Fraga anababatizana na mchezaji wa Mtibwa, mpira unakwena nje, unarushwa kuelekea Mtibwa. Dak ya 42, Tayari Shiboub alishaamka, na zikiwa zimesalia dakika mbili mpira kwenda mapumziko. Dak ya 41, Shiboub anafanyiwa madhambi, na mpira umesimama kwa muda. Dak ya 38, Kanoni anatolewa nje na machela baada ya kuumia, matokeo bado ni 1-1. Dak ya 37, Chamaaaaa, pata nafasi moja maridadi kabisa lakini shuti lake linakwenda moja kwa moja kwa Kado kwa kulidaka. Dak ya 33, Inapigwa lakini inakwenda moja kwa moja kwa Manula ambaye anapangua na kuuelekeza eneo la kati mwa uwanja. Dak ya 32, Mtibwa wanapata faulo, anakwenda kupiga Salum Kanoni, piga mkwaju mkali unapanguliwa na Manula, inakuwa kona. Dak ya 31, Mtibwa wanajichanganya eneo lao la ulinzi, Simba wanaudaka kwake Kagere, bahati si yake. Kipa anadaka. Dak ya 30, ni kona nyingine inapigwa kuelekezwa Mtibwa, anapiga Chama, piga kule lakini inababatizwa na wachezaji wa Simba, golikiki. Dak ya 28, Mpira umesimama kwa muda, mchezaji wa Mtibwa ameumia. Dak ya 27, Offside kwa, mpira unachezwa na Mtibwa. Dak ya 25, Kapombe anapasiana na Chama eneo la kati mwa Uwanja, maelewano yanakuwa si mazuri, na mpira unakuwa golikiki, unaelekezwa Simba. Dak ya 24, Mpira unarushwa kuelekea lango la Mtibwa, ni karibu na eneo la kona, umesharushwa na unatolewa tena. Dak ya 21, Rifat Hamis anaisawazishia Mtibw aSugar kwa mpira wa kichwa ulitokana na kona, ni 1-1. Dak ya 17, Goooli, Meddie Kagere anafunga bao la kwanza baada ya Simba kupasiana vema katika eneo la hatari, sasa ni 1-0. Dak ya 10, Golikiki imetokea upande wa Simba, wanaanza upya kwake Manula. Dak ya 9, Simba wanapata kona ya kwanza,wanapiga lakini inatolewa nje na Mtibwa, wanaenda kurusha, Chama anarusha. Dak ya 7, Simba wanatandaza pasi nzuri kuelekea Mtibwa, kwake Shomari Kapombe, anapiga krosi ambayo inashindwa kuzaa matunda. Dak ya 6, Kado anaokoa mpira uliopigwa na Chama akiwa peke yake, ni nafasi ambayo Simba wamngeshaandika bao. Dak ya 6, Bado Simba wanaonekana kuutawala mchezo zaidi ya Mtibwa kwa dakika hizi sita za mwanzo. Dak ya 4, Simba wanaanza faulo kwa kupasiana, anapiga Nyonii, inaokolewa na mabeki wa Mtibwa. Dak ya 3, Zimbwe Jr anakokotoa mpira na guu la kushoto kushoto mwa uwanja, mchezaji Awadhi Salum wa Mtibwa anashikana mkono, faulo. Dak ya 3, Manula anadaka mpira, anaanzisha mashambulizi upya. Dak ya 2, Rifat Hamis wa Mtibwa anapandisha mashambulizi kwenda Simba, ni la kwanza. Dak ya 1, mechi imeshaanza Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, na Simba wameanza kwa kushambulia kwa kasi lango la Mtibwa. Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/Kidanistars



Msanii JB: Tutaenda 'Kombe la Dunia' Tukutane Taifa Kesho
Msanii JB: Tutaenda 'Kombe la Dunia' Tukutane Taifa Kesho

Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/Kidanistars



Ibrahim Ajibu Afunguka Simba Kuwafunga JKT Tanzania
Ibrahim Ajibu Afunguka Simba Kuwafunga JKT Tanzania

Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/Kidanistars



Kocha Jkt Tanzania: Simba Katufunga Kizembe, Auzunika
Kocha Jkt Tanzania: Simba Katufunga Kizembe, Auzunika

Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/Kidanistars



Simba Watua Taifa Kibabe Kuwafunga Jkt Tanzania, Ligi Kuu
Simba Watua Taifa Kibabe Kuwafunga Jkt Tanzania, Ligi Kuu

Subscribes:https://www.youtube.com/c/KidaniStars MABINGWA watetezi, Simba SC wameanza vyema msimu mpya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya JKT Tanzania Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam. Mshambuliaji wa kimataifa wa Rwanda, Meddi Kagere alikaribia kufunga hat trick katika mechi ya kwanza baada ya kufunga mabao mawili, huku lingine likifungwa na Miraj Athumani ‘Madenge’ aliyerejeshwa kikosini msimu huu. Instagram: https://www.instagram.com/kidanistars Simba SC: Aishi Manula, Haruna Shamte, Mohammed Hussein, Erasto Nyoni, Tairone Santos, Gerson Fraga, Deogratius Kanda/Miraj Athumani dk60, Muzamil Yassin, Meddie Kagere, Hassan Dilunga/Sharaf Shiboub dk71 na Clatous Chama/Ibrahim Ajibu dk78. Facebook: https://www.instagram.com/kidanistars Twitter: https://twitter.com/Kidanistars




« Previous Next »


User Detail Page

You can find user latest posts and related content on the page. Friends, comments for events / matches are also available on the page. Even you can find users who are same pleasure with current user.

#Travel, #SupportYourTeam, #AllAboutSports