Timu ya Mtibwa Sugar leo imefanikiwa kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mwadui FC, goli pekee likifungwa na Riphat Khamis Msuya dakika ya 7. Ni mechi ya ligi kuu Tanzania Bara iliyochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro. Tufuatilie kwenye mitandao mingine ya kijamii:- ►INSTAGRAM: https://www.instagram.com/azamtvtz/ ►INSTAGRAM: https://www.instagram.com/azamsports2/ ►TWITTER: https://twitter.com/azamtvtz ►FACEBOOK: http://www.facebook.com/azamtvtz ►WEBSITE: http://www.azamtv.co.tz
Hatimaye wakata miwa wa Mtibwa, timu ya Mtibwa Sugar wamepata ushindi wa kwanza baada ya takriban mechi nane za ligi kuu Tanzania Bara, wakiichapa Coastal Union mabao 3-1 kwenye uwanja wa Manungu, mkoani Morogoro. Coastal ndiyo waliotangulia kupata bao kupitia kwa Ayoub Lyanga dakika ya 21, lakini wenyeji Mtibwa wakasawazisha kupitia kwa Dickson Daud dakika ya 40, kabla ya Jaffary Kibaya kupachika bao la pili dakika ya 55 na Riphat Khamis dakika ya 67. Ushindi huo umeifanya Mtibwa ipande juu kwa nafasi sita kutoka nafasi ya 17 hadi ya 11 baada ya kufikisha pointi 32.
Timu ya Mtibwa Sugar imeendelea kupokea vipigo kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya leo kufungwa mabao 2-1 na Biashara United kwenye Uwanja wa Karume mjini Musoma. Wenyeji Biashara United ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 39 kupitia kwa George Makang’a kwa mpira wa adhabu ndogo ‘free-kick’, lakini Mtibwa walisawazisha kupitia kwa kichwa cha Riphat Kamis dakika ya 64 na kisha Biashara kupata bao la ushindi dakika ya 80 kupitia kwa Innocent Edwin.
Timu ya Mtibwa Sugar imeendelea kupokea vipigo kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya leo kufungwa mabao 2-1 na Biashara United kwenye Uwanja wa Karume mjini Musoma. Wenyeji Biashara United ndiyo waliotangulia kupata bao dakika ya 39 kupitia kwa George Makang’a kwa mpira wa adhabu ndogo ‘free-kick’, lakini Mtibwa walisawazisha kupitia kwa kichwa cha Riphat Kamis dakika ya 64 na kisha Biashara kupata bao la ushindi dakika ya 80 kupitia kwa Innocent Edwin. Tazama mabao.
Timu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imeanza vyema michuano ya Afrika kwa kuichapa Northern Dynamo mabao 4-0 katika mchezo wa hatua ya awali wa Kombe la Shirikisho barani Afrika. Katika mchezo huo uliopigwa kwenye Dimba la Azam Complex Chamazi, mshambuliaji wa Mtibwa Jaffary Salum Kibaya ameibuka shujaa kwa kupigwa hat-trick, akifunga mabao yake katika dakika za 13, 36 na 58 huku bao la nne likifungwa na Riphat Khamis aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ismail Mhesa. Kwa matokeo haya, mtibwa wamejiweka pazuri katika njia kusonga mbele kwani watahitaji sare ya aina yoyote ili kufuzu hatua inayofuata au wasifungwe mabao zaidi ya matatu.
Timu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro imeanza vyema michuano ya Afrika kwa kuichapa Northern Dynamo mabao 4-0 katika mchezo wa hatua ya awali wa Kombe la Shirikisho barani Afrika. Katika mchezo huo uliopigwa kwenye Dimba la Azam Complex Chamazi, mshambuliaji wa Mtibwa Jaffary Salum Kibaya ameibuka shujaa kwa kupigwa hat-trick, akifunga mabao yake katika dakika za 13, 36 na 58 huku bao la nne likifungwa na Riphat Khamis aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ismail Mhesa. Kwa matokeo haya, mtibwa wamejiweka pazuri katika njia kusonga mbele kwani watahitaji sare ya aina yoyote ili kufuzu hatua inayofuata au wasifungwe mabao zaidi ya matatu.