DAR DERBY: Yanga SC imeangukia pua kwa kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Azam FC, katika #DarDerby iliyopigwa leo Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Yanga imetangulia kupata bao kupitia kwa Clement Mzize dakika ya 10 kabla ya Azam kuchomoa dakika ya 19 kwa goli la Gibril Sillah na kisha Feisal Salum akafunga la ushindi dakika ya 51.
DAR DERBY: Yanga SC imeangukia pua kwa kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Azam FC, katika #DarDerby iliyopigwa leo Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. Yanga imetangulia kupata bao kupitia kwa Clement Mzize dakika ya 10 kabla ya Azam kuchomoa dakika ya 19 kwa goli la Gibril Sillah na kisha Feisal Salum akafunga la ushindi dakika ya 51.
Clatous Chama amefunga magoli mawili muhimu dakika ya 57 na 73, Simba ikipata ushindi wa 2-0 dhidi ya Mashujaa FC, mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa #AzamComplex, Chamazi .
Stephane Aziz Ki ametoa 'assist' tatu na kufunga goli moja, Yanga ikiichakaza Ihefu kwa kichapo cha mabao 5-0, mchezo wa ligi kuu ya NBC #NBCPremierLeague kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi. Aliyefungua Dimba alikuwa ni Pacome Zouzoua dakika ya 10, Mudathir Yahya dakika ya 30, Aziz Ki dakika ya 68, Augustine Okrah dakika ya 84 na Maxi Nzengeli dakika ya 86.
Stephane Aziz Ki ametoa 'assist' tatu na kufunga goli moja, Yanga ikiichakaza Ihefu kwa kichapo cha mabao 5-0, mchezo wa ligi kuu ya NBC #NBCPremierLeague kwenye Dimba la Azam Complex, Chamazi. Aliyefungua Dimba alikuwa ni Pacome Zouzoua dakika ya 10, Mudathir Yahya dakika ya 30, Aziz Ki dakika ya 68, Augustine Okrah dakika ya 84 na Maxi Nzengeli dakika ya 86. Haya hapa magoli yote matano....
Simba SC imechezea kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Tanzania Prisons, katika mchezo wa ligi kuu ya NBC uliopigwa kwenye Dimba la Jamhuri, Morogoro. Magoli yote mawili ya Tanzania Prisons yamefungwa na Samson Mbangula dakika ya 45 na 62 huku goli pekee la Simba likipatikana dakika ya 89 kupitia kwa Fabrice ngoma. Tazama Highlights....
Hizi hapa hekaheka za Selemani Kidunda na Asemahle kwenye pambano lao la raundi 12. Pambano hili limemalizika bila mshindi yaani droo.
Tazama matukio yote muhimu yaliyojiri kwenye mechi ya Azam Sports Federation Cup kati ya Simba SC dhidi ya TRA Kilimanjaro. Magoli matatu yamefungwa na Sadio Kanoute, wengine ni Pa Omar Jobe, Fredy Michael Koublan na Ladack Chasambi